pmbet

Mungu hapokei maombi ya viongozi wanaonzisha vita - Papa Leo

Eric Buyanza

March 30, 2026
Share :

Huku mzozo katika Mashariki ya Kati ukiendelea, Kiongozo wa Kanisa Katoliliki Duniani Papa Leo XIV ameonekana kuwakosoa wale wanaohusika na vita hivyo.

 

Akiwahutubia waumini wa kanisa hilo mjini Vatican wakati wa maadhimisho ya Jumapili ya Mitende, Papa alisema Mungu anakataa maombi ya viongozi wanaoanzisha vita na kuwa na "mikono iliyojaa damu", katika kile ambacho kimetafsiriwa kuwa ukosoaji wa wale waliohusika katika vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran.
 

"Huyu ndiye Mungu wetu: Yesu, mfalme wa amani, anayekataa vita, ambaye hakuna mtu anayeweza kumtumia kuhalalisha vita," anasema Papa.

"Hasikii maombi ya wapiganaji, lakini anakataa." Akinukuu kifungu fulani cha Biblia, anasema: “‘Hata mjaposali sala nyingi, sitasikiliza: mikono yenu imejaa damu’.”


 


 

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet