pmbet

Mwanafunzi ashambulia wenzake kwa risasi

Eric Buyanza

April 3, 2024
Share :

Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 12 amefariki na wengine wawili wamejeruhiwa baada ya mwanafunzi mwenzao kuwashambulia kwa bunduki ndani ya shule kusini mwa Finland Jumanne.

Shambulizi hilo limetokea katika mji wa Vantaa wakati masomo yakiendelea.

Mshukiwa huyo aliyeshambulia kwa bunduki, ametambuliwa kuwa ni mwanafunzi mwenye umri wa miaka 12, aliyekimbia kwa miguu na baadae kukamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi.

Mwaka 2007, Pekka-Eric Auvinen mwenye umri wa miaka 18 aliwashambulia kwa bunduki watu tisa, wakiwemo wanafunzi wenzake sita, katika Shule ya Sekondari ya Jokela iliyoko karibu na Helsinki kabla ya kujiua yeye mwenyewe kwa kujipiga risasi.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet