Mwanamke mbaroni kwa kumiliki gereza lake mwenyewe
Eric Buyanza
December 10, 2025
Share :
Huko kwenye mji wa NkowaNkowa jimbo la Limpopo nchini Afrika ya Kusini, mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 54 anashikiliwa na polisi akituhumiwa kufungua gereza lake mwenyewe.
Mwanamke huyo anayemiliki kilabu kidogo cha pombe alifungua gereza hilo nyuma ya nyumba yake na alikuwa akiwakamata na kuwasweka ndani wanaume kadhaa waliokuwa wakisababisha vurugu wakiwa wamelewa na wale ambao walikuwa wameshindwa kulipa bili ya pombe walizokunywa kwenye kilabu hicho.
Kulingana na ripoti ya polisi, mwanamke huyo alikuwa akiwashikilia wanaume 36 kwa kunywa pombe na kushindwa kulipa bili.






