Mwenyekiti Simba ameenda kuhani kwa Rais Samia
Eric Buyanza
September 10, 2026
Share :
Mwenyekiti wa Simba Murtaza Mangungu ameungana na Watanzania wengine waliokwenda nyumbani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kufuatia kifo cha Mume wake Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan aliyefariki dunia September 07, 2026.
Mangungu amekwenda Visiwani Zanzibar, Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, kumfariji Rais Samia.






