Natamani kukutana na kiongozi wa Iran Mojtaba Khamenei - Trump
Eric Buyanza
June 4, 2026
Share :

Rais wa Marekani Donald Trump amesema angependa kukutana na Kiongozi Mkuu wa Iran, Mojtaba Khamenei.
Ameyesama hayo jana (Jumatano) katika mahojiano na Gazeti la New York Post.
"Ningependa kukutana nae, Wairan wanamheshimu sana," alisema Rais Donald Trump na kuongeza...”Ningependa kukutana na viongozi wote wa Iran, na pengine tutakutana, kulingana na kitakachotokea," alimalizia.
Kiongozi huyo mpya bado hajaonekana hadharani nchini Iran tangu kuteuliwa kwake baada ya kifo cha baba yake katika mashambulizi ya anga yaloyotekelezwa na Marekani na Israel mwishoni mwa mwezi Februari.





