Neymar Jr akutwa na jeraha jipya akiwa Timu ya Taifa.
Joyce Shedrack
May 28, 2026
Share :
Madaktari wa timu ya Taifa ya Brazil wamethibitisha kuwa mshambuliaji Neymar Jr alipata uvimbe wa daraja la pili kwenye misuli (grade 2 calf edema) wakati wa mechi ya Santos FC na kutokana na jeraha hilo, anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa wiki mbili hadi tatu.

Ingawa atakosa mechi za kirafiki za maandalizi dhidi ya Panama na Misri, bado ameendelea kujumuishwa katika kikosi rasmi cha wachezaji 26 cha kocha Carlo Ancelotti kwa ajili ya Kombe la Dunia 2026.





