"Nimehuzunika,Nimeumia lakini ndoto bado inaishi"Neymar Jr.
Joyce Shedrack
March 17, 2026
Share :
Mshambuliaji wa Timu ya Taifa ya Brazil na Klabu ya Santos Neymar Jr amefunguka baada ya kutojumuishwa kwenye kikosi cha Timu yake ya Taifa kitakachocheza mechi 2 za kirafiki kujiandaa na Kombe la Dunia 2026.

Neymar ameweka wazi kuwa ameumizwa kukosekana kwenye kikosi hicho kilichoitwa na Carlo Ancelotti huku akisema kuwa bado kuna nafasi moja ya mwisho.
“Nimehuzunika, nimeumia lakini ninalenga kabisa kila siku mazoezi baada ya mazoezi, mchezo baada ya mchezo kwa sababu bado kuna nafasi moja ya mwisho, NDOTO BADO INAISHI na tutaifikia lengo letu!”, amesema Neymar Jr .





