"Nimemwambia Perez amsajili Olise yupo kama Messi"-Makelele.
Joyce Shedrack
July 17, 2026
Share :
Nguli wa soka la Ufaransa aliyewahi kuichezea Real Madrid, Claude Makélélé amefichua kuwa alimshauri rais wa klabu hiyo, Florentino Pérez kufanya kila linalowezekana kumsajili nyota wa Kifaransa Michael Olise.

Makélélé amesema anaamini Olise ni miongoni mwa vipaji vya kipekee vinavyoweza kubadili mchezo kwa ubora wake akimfananisha na gwiji Lionel Messi kutokana na uwezo wake wa kufanya mambo yasiyotegemewa uwanjani.
"Yupo kama Messi, anaweza kufanya kitu ambacho hakuna anayetarajia ndiye mchezaji wa karibu zaidi tuliyenaye kwa Ronaldo Nazário,"
"Nilimwambia Florentino Pérez kwamba kama angeamua kutumia fedha kwa mchezaji mmoja, basi angepaswa kumsajili Michael Olise," amesema Makelele.





