Niyonzima kuagwa kwa heshima Rwanda
Sisti Herman
March 16, 2026
Share :

Kiungo mshambuliaji wa zamani wa Simba na Yanga, Haruna Niyonzima atastaafu rasmi soka baada ya msimu huu kumalizika.
Kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Rwanda (FERWAFA), Niyonzima anayechezea AS Kigali, kwa sasa amekuwa katika mchakato wa kuandaa mechi ya kumuaga rasmi ambayo itashirikisha mastaa wa soka wa nchi hiyo.
Mbali na Simba na Yanga, Niyonzima amewahi pia kuzitumikia APR, Rayon Sports za Rwanda.





