pmbet

Nyundo na wenzake waomba hukumu, kesi kufutwa

Sisti Herman

June 11, 2025
Share :

 

Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma imeendelea kusikiliza hoja za rufaa kupinga kifungo cha Maisha jela walichohukumiwa aliyekuwa askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Clinton Damas, maarufu Nyundo na wenzake Amin Lema, Nickson Jackson na aliyekuwa Askari Magereza, Praygod Mushi, huku upande wa Jamhuri ukiomba kuzijibu Juni 12, 2025
-
Akiwasilisha hoja Mahakamani, Juni 10, 2025, Wakili wa Warufani hao, Godfrey Wasonga amedai kulikuwa na dosari za Kisheria katika kesi hiyo kuanzia hati ya mashtaka hadi hukumu. Amedai Mahakama ilioneshwa vipande Vinne vya Video ambavyo ni 6, 7, 8 na 9 lakini kwenye hukumu, vipande vya Video vilivyowatia hatiani ni namba 1, 2, 3 na 4 ambavyo havikuoneshwa Mahakamani hapo
-
Aidha, kwa mujibu wa Wakili huyo, vipande vya Video vilivyooneshwa viliwaonesha washtakiwa wakijirekodi wakiwa wanacheza Muziki, huku wakiwa na chupa za Vinywaji lakini hazikuonesha wakiwa wanatenda kosa la kubaka kwa kikundi wala kulawiti

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet