Osuri aongoza Mkutano Mkuu wa chama cha soka Simiyu
Sisti Herman
February 7, 2026
Share :

Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Mkoa wa Simiyu Ndugu OSURI KUSURI akiwa katika Usimamizi na Uendeshaji wa Kikao cha Mkutano Mkuu wa Kawaida wa Chama hicho kwa mujibu wa Katiba yake na chini ya Miongozo ya TFF.
Moja ya mambo muhimu aliyoweka Mkazo katika kikao hicho ni kuweka msisitizo na mikakati ili Vyama vya Soka vya Wilaya viwe hai na kuweza kufanya kazi zake bila kusahau jambo kubwa sana kufanya Mikutano ya Kikatiba.
Mwisho aliwapa wajumbe wote salamu toka kwa Rais wa Soka Tanzania (TFF) Ndugu Wallace Karia na kwa pamoja amemshukuru Rais kwa msaada mkubwa anaotoa kwa Chama cha Mkoa wa Simiyu na kumpa pongezi za dhati kwa mambo makubwa yanayoelezeka anayoendelea kuyafanya kwa Taifa hili kwa Ujumla.





