pmbet

Pederan anyongwa leo Iran, kwa kutoa siri za jeshi kwa Israel

Eric Buyanza

September 19, 2026
Share :

Mahakama nchini Iran imetangaza rasmi kumnyonga Hossein Pedaran, raia wa nchi hiyo aliyepatikana na hatia ya kufanya ujasusi kwa niaba ya Israel.

Hukumu hiyo imetekelezwa leo Jumamosi, Septemba 19, 2026 baada ya kutupilia mbali rufaa zote za mshtakiwa.

 

Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na shirika la habari la Idara ya Mahakama, Mizan News Agency, Pedaran alitiwa mbaroni na maafisa wa usalama wa Iran baada ya ufuatiliaji wa muda mrefu wa kijasusi.

 

Mahakama imeeleza kuwa mshtakiwa alikuwa akishirikiana kwa karibu na maafisa wa Mossad kwa lengo la kuujeruhi usalama wa taifa la Iran.

Pedaran anatuhumiwa kukusanya na kusafirisha taarifa za siri zilizohusu kambi za kijeshi na maghala ya makombora katika mkoa wa Isfahan.

Mbali na ramani za maeneo hayo, alitoa wasifu na taarifa binafsi za wataalamu na wafanyakazi wanaohudumu katika vituo hivyo vya ulinzi.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet