Pitso awasha taa ya kijani kujiunga na Pyramids
Sisti Herman
June 11, 2026
Share :

Kocha raia wa Afrika Kusini Pitso Mosimane amependezwa na mradi wa kuchukua mikoba ya kuinoa Pyramids FC kwa 100% na ametoa taa ya kijani kuashiria kuwa yupo tayari kupewa majukumu.
Sasa, 'mpira' uko kwenye uwanja wa Pyramids. Uongozi wa klabu kwa sasa uko katika majadiliano ya ndani, wakichunguza pendekezo hilo kabla ya kuandaa nyaraka rasmi na kufanya uamuzi wao wa mwisho.
Bado hakuna kibali rasmi au kukataliwa kilichotumwa, lakini Mosimane anasubiri.





