Pitso Mosimane rasmi ni kocha Mkuu wa Afrika Kusini.
Joyce Shedrack
September 1, 2026
Share :
Shirikisho la Soka la Afrika Kusini (SAFA) limemtangaza Pitso Mosimane kuwa kocha mkuu mpya wa timu ya taifa ya Afrika Kusini, Bafana Bafana.
Mosimane, ambaye ni miongoni mwa makocha wenye uzoefu mkubwa barani Afrika, anatarajiwa kuiongoza timu hiyo pamoja na kikosi chake cha benchi la ufundi katika majukumu mbalimbali ya kimataifa.
Uteuzi huo unalenga kuimarisha Bafana Bafana na kuhakikisha timu hiyo inapata mafanikio katika mashindano yajayo, huku Mosimane akipewa jukumu la kutumia uzoefu wake kujenga timu yenye ushindani.
SAFA pia imetangaza timu ya wataalamu watakaoshirikiana na Mosimane katika benchi la ufundi, kwa lengo la kuhakikisha maandalizi ya timu yanafanyika kwa kiwango cha juu.





