Pochettino kuitazama Tottenham baada ya mashabiki kutaka arudi
Eric Buyanza
March 10, 2026
Share :
Kocha wa timu ya taifa ya Marekani USA, Mauricio Pochettino, anatarajiwa kuangalia mechi ya timu yake ya zamani, Tottenham, dhidi ya Atletico Madrid usiku wa leo kwenye Ligi ya Mabingwa barani Ulaya.
Pochettino atakuwa mgeni wa Atletico Madrid kwenye uwanja wa Metropolitano.
Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Pochettino kuangalia mechi ya Tottenham tangu aondoke klabuni hapo mwaka 2019. Pochettino amehusishwa na kurudi Tottenham kama kocha mkuu, hasa baada ya Thomas Frank kuondolewa kwenye nafasi hiyo.





