"Presha ni kubwa kwetu kwa sababu tuko nyumbani"Walid Regragui.
Joyce Shedrack
January 17, 2026
Share :
Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Morocco Walid Regragui akizungumza kuelekea mchezo wa Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON 2025 dhidi ya Senegal amekiri ni kweli wana presha kubwa kuelekea mchezo huo.

“Presha ni kubwa kwetu Morocco kwa sababu tunacheza nyumbani hivyo tunapaswa kudhibiti hisia zetu, mechi dhidi ya Tanzania hatukuweza kufunga goli katika dakika 25 za kwanza, mechi ya Cameroon ilikuwa ni ya mtoano pia tukalazimika kubadilika na hii ni fainali ni muhimu kubadilika maana tunacheza na timu inayojiamini sana na wamekuwa na muendelezo mzuri”Amesema Walid Regragui.
Mchezo huo utapigwa kesho katika dimba la Prince Moulay Abdellah kuanzia saa 4:00 usiku.





