Raia 62 wa Ghana wauawa na Ukraine wakiipigania Urusi
Eric Buyanza
August 19, 2026
Share :

Waziri wa mambo ya nje wa Ghana Samuel Okudzeto Ablakwa, amesema raia 62 wa nchi hiyo wameuawa wakiipigania Urusi katika vita vya Ukraine huku wengine 15 wakiwa hawajulikani waliko.
Bwana Ablakwa ambaye yuko Moscow kwa mazungumzo na mwenzake wa Urusi Sergei Lavrov, amewaambia waandishi wa habari kuwa kusajiliwa kwa raia wa mataifa ya kiafrika kupigana katika vita kati ya Urusi na Ukraine kunapaswa kukoma.
Kulingana na maafisa wa Ukraine, zaidi ya Waghana 272 wamesajiliwa na Urusi tangu mwaka 2022.
Ukraine inasema takriban Waafrika 2,000 kutoka mataifa 36 ya Kiafrika wanapigana kwa niaba ya Urusi.
Maafisa wa Urusi wanakanusha kuwa wanawasajili waafrika kinyume na sheria.
BBC





