Rais Kiir amteua 'marehemu' kwenye kamati ya uchaguzi
Eric Buyanza
February 4, 2026
Share :
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amemteua bila kukusudia mtu aliyekufa kuwa mjumbe wa kamati itakayoandaa uchaguzi wa nchi hiyo.
Akiweka mambo sawa, msemaji wa ofisi ya rais alisema kwamba mamlaka zilipitiwa wakati wa uteuzi baada ya Steward Sorobia Budia, mwanasiasa wa zamani wa upinzani aliyefariki miaka 5 iliyopita kuwa miongoni mwa wajumbe waliotajwa kwenye teuzi hizo.
DW






