Rais Yanga achukua fomu ya Ubunge Kigamboni
Eric Buyanza
June 28, 2025
Share :
Rais wa Yanga SC, Mkandarasi Hersi Said amechukua Fomu ya kuwania Ubunge katika Jimbo la Kigamboni lililopo Jijini Dar es Salaam.
Hersi mwenye ushawishi mkubwa katika masuala ya soka amechukua fomu hiyo leo kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).
Ikumbukwe Jimbo hilo liliondokewa na aliyekuwa Mbunge wake Faustine Ndugulile aliyefariki dunia mwanzoni mwa mwaka huu alipokuwa nchini India kwa ajili ya matibabu.