Rapa 50 Cent atoa povu kisa P Diddy kuachiliwa mapema gerezani.
Joyce Shedrack
June 17, 2026
Share :
Rapa maarufu 50 Cent ameendelea kumkejeli mpinzani wake wa muda mrefu Sean Combs baada ya taarifa kuonyesha kuwa muda wake wa kifungo unaweza kupunguzwa.

Kwa mujibu wa kauli zake za hivi karibuni, 50 Cent anaamini Diddy anaweza kuachiliwa mapema, lakini amesema hilo halimaanishi kwamba tabia zake zitabadilika.
50 Cent alisema kuwa anaamini Diddy “atarudi nyumbani mapema,” lakini akaongeza kuwa muda mfupi gerezani huenda usitoshe kumfanya abadili mwenendo wake.
Kauli hiyo imezua mjadala mkubwa mtandaoni kutokana na ugomvi wao wa muda mrefu.





