Real Madrid yajiondoa kwenye vita ya kusaka saini ya Julian Alvarez.
Joyce Shedrack
June 19, 2026
Share :
Klabu ya Real Madrid imejiondoa rasmi kwenye dili la Julián Álvarez baada ya pendekezo la euro milioni 150 kukataliwa wiki iliyopita.
Real Madrid hawakurudi tena kwenye mazungumzo, na vyanzo vya Atlético vinaamini kwamba ilikuwa ni mbinu ya kujifanya ya Florentino Pérez si lengo la kweli walilokuwa wakilifuatilia.
Vyanzo vinaamini kuwa Real Madrid waliondoka kwenye mchakato huo kwa sababu Florentino alikuwa na wazo moja nyota mkubwa pekee aliyemtaka kwa dhati alikuwa Michael Olise. Ndiye jina lililotamaniwa zaidi na Pérez nyuma ya pazia.
Bayern Munich hawataki kumuuza Olise na wanazingatia kumpa mkataba mpya, lakini nyota huyo alikuwa akitamaniwa zaidi na Florentino alikuwa Olise.





