Real Madrid yamtambulisha Ibrahim Konate.
Joyce Shedrack
June 18, 2026
Share :
Klabu ya Real Madrid imemtangaza mlinzi wa kati, lbrahima Konaté kama mchezaji mpya klabuni hapo akikamilisha uhamisho huru akitokea Liverpool baada ya mkataba wake na majogoo hao kutamatika mwisho wa msimu wa 2025/26.
Real Madrid imethibitisha usajili huo siku ya leo kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii ambapo Konaté raia wa Ufaransa amesaini mkataba wa miaka minne utakaombakisha klabuni hapo mpaka Juni 2030.





