Saha amshauri Carrick kumsajili Vini Jr
Sisti Herman
February 16, 2026
Share :

Aliyekuwa mshambuliaji wa Manchester United, Louis Saha, anaamini kuwa nyota wa Real Madrid, Vinícius Júnior, anaweza kushawishika kujiunga na Old Trafford huku akimshauri kocha wa muda wa timu hiyo kumjumisha kikosini endapo atapewa kazi rasmi.
Saha amedokeza kuwa licha ya mafanikio ya Mbrazili huyo nchini Uhispania, changamoto ya kuirudisha United katika enzi zake za utukufu pamoja na mvuto wa Ligi Kuu ya Uingereza huenda vikamtosha winga huyo kukubali uhamisho wa kushtua.





