Salah atumiwa ofa kutoka Saudia
Sisti Herman
February 11, 2026
Share :

Klabu ya Al-Ittihad imeanza rasmi mazungumzo na nyota wa Liverpool, Mohamed Salah, ili kumshawishi kujiunga nao msimu ujao wa majira ya joto.
Mabingwa hao wa Saudi Arabia wanaonekana kudhamiria kumnasa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Misri kama sehemu ya mkakati wao wa kuimarisha kikosi chao kwa mastaa wakubwa duniani.
Ingawa Salah bado ni mchezaji muhimu ndani ya Anfield, ofa hiyo kutoka Mashariki ya Kati inasemekana kuwa nono na yenye kuvutia, jambo linalozua maswali kuhusu mustakabali wake nchini Uingereza.





