Saudi Arabia yazuia makombora 8 yaliyotumwa Riyadh
Eric Buyanza
March 23, 2026
Share :

Vikosi vya anga vya ulinzi vya Saudia vilinasa makombora 8 ya balestiki yaliyorushwa kuelekea mji wa Riyadh, Wizara ya Ulinzi ya nchi hiyo ilitangaza.
Wizara ilisema kwenye jukwaa la kijamii la X kwamba makombora manne ya balistiki yaliyorushwa kuelekea Riyadh yalinaswa na kuharibiwa, na “sehemu ya kombora moja la balistiki lilianguka karibu na kiwanda cha kusafisha mafuta kusini mwa Riyadh.”
Mapema siku ya Jumatano, ilisema makombora manne ya balistiki yaliyorushwa kuelekea Riyadh yalinaswa na kuharibiwa, huku vifusi vikianguka katika maeneo mbalimbali ya mji mkuu.
Wakati huo huo, Ulinzi wa Raia wa Saudia umesema kuwa wakaazi wanne wamejeruhiwa na uharibifu mdogo wa nyenzo ulisababishwa baada ya vifusi vya kombora la balestiki kuangukia kwenye makazi ya watu huko Riyadh.
Tukio hilo linakuja huku kukiwa na mvutano mkubwa wa kikanda kufuatia wiki kadhaa za kuongezeka kwa mabadilishano kati ya Iran na muungano wa Marekani na Israel.





