Senegal yaingiza kombe la AFCON 2025 na taulo uwanjani
Sisti Herman
March 29, 2026
Share :

Timu ya Taifa ya Senegal jana ilingia uwanjani na kombe lao la AFCON 2025 wakati wa mchezo wa kirafiki dhidi ya Peru uliochezwa nchini Ufaransa.
Wakati taji hilo lipo jukwaani, taulo lilionekana karibu na kombe hilo, wengi wakitafsiri kama utani kwa timu ya taifa ya Morocco waliokuwa maarufu kwenye michuano ya AFCON 2025 kwa kupora mataulo ya makipa wa wapinzani wao





