Siku ya kihistoria kwenye soka la Tanzania.
Joyce Shedrack
June 2, 2026
Share :
Timu ya Taifa ya Wanaume chini ya umri wa miaka 17 @serengetiboystz siku ya leo majira ya saa 4 usiku inatarajia kushuka uwanjani majira ya saa 4 usiku kucheza mchezo wa Fainali ya michuano ya AFCON U17 dhidi ya Senegal.

Serengeti Biys ambao wamekuwa na ubora mkubwa kwenye michuano hiyo wamefanikiwa kutinga fainali baada ya kuiondosha Misri kwenye Nusu Fainali kwa mikwaju ya penalti huku wakiwa na safari ya kuvutia wakiwa wamepoteza mchezo mmoja pekee hadi ya hatua hiyo.
Katika mechi mechi 5 walizocheza mpaka sasa kuanzia hatua ya makundi wameshinda michezo minne wakipoteza mchezo mmoja tu wa hatua ya makundi kwa mabao 2-1 dhidi ya Mali.





