pmbet

Simba, Yanga zakabidhiwa timu toka Kilimanjaro

Joyce Shedrack

February 2, 2024
Share :

Droo ya kombe la Shirikisho la Azam Sport Federation Cup raundi ya 16 imefanyika  hii leo huku timu zilizofuzu raundi hiyo zikimjua mshindani wa kwenda kucheza naye hatua inayofuata, vigogo wa soka la Tanzania Simba sc na Yanga SC  zimepangiwa kukutana na timu za Mkoa wa Kilimanjaro.

 

Simba sc amepangwa na bingwa wa Mkoa huo TRA Kilimanjaro FC na bingwa mtetezi wa kombe hilo Young Africans SC imepangwa kucheza na Polisi Tanzania, Azam FC itakutana  na Green Worriors .

 

Timu zingine zitakazo kutana hatua hii baada ya kuchezwa kwa michezo ya hatua ya 32 bora  ni :
 

Singida FG vs FGA Talents, 

Tabora United VS Nyamongo FC,

Mtibwa Sugar VS Stand United

Ihefu SC VS Mbuni FC

JKT Tanzania VS TMA FC

Kagera Sugar VS Pamba FC

Rhino Rangers VS Mabao FC

Geita Gold VS Mbeya City 

Namungo VS Transit Camp

Dodoma Jiji VS Biashara UTD

Coastal Union VS Mbeya Kwanza

KMC VS Gunners

Mashujaa FC VS Mkwajuni FC.

 

Michezo hiyo imepangwa kucheza kati ya Februari 19 na 20 mwaka huu kwa mujibu wa Kalenda.

Mshindi wa michezo hiyo atakuwa amekata ticket ya kuingia robo fainali ya michuano hiyo ambayo bingwa mtetezi ni Yanga SC aliyechukua kombe msimu jana katika fainali iliyowakutanisha na matajiri wa Chamazi Azam FC wananchi walichukua kombe hilo kwa ushindi wa bao moja kwa sifuri dhidi ya Azam FC.

 

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet