Simba yaruhusiwa kufanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja wa B.Mkapa.
Joyce Shedrack
June 13, 2025
Share :
Klabu ya @simbasctanzania imepokea barua ya kuruhusiwa na Wizara ya Habari Utamaduni,Sanaa na Michezo kufanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja wa Benjamini Mkapa kwa ajili ya mchezo wa Kariakoo Derby utakaochezwa siku ya jumapili Juni 15 mwaka huu.
Kikosi cha Simba kitafanya mazoezi ya mwisho katika uwanja huo siku ya jumamosi juni 14.