Sitairuhusu Iran kuwa na silaha za nyuklia - Trump
Eric Buyanza
February 25, 2026
Share :

Rais wa Marekani Donald Trump ametoa hotuba yake ya kila mwaka katika majengo ya Bunge la Marekani na kusisitiza kuwa hatoiruhusu Iran kuwa na silaha za nyuklia.
Rais wa Marekani amesema: "Kwa miongo kadhaa, imekuwa sera ya Marekani kutoruhusu Iran kupata silaha za nyuklia.”
“Wameonywa wasijaribu kujenga upya mpango wao wa silaha, lakini wanaendelea. Napenda tutatue tatizo hili kupitia diplomasia, lakini jambo moja ni hakika: Sitawaruhusu kupata silaha za nyuklia."
Trump ameweka rekodi ya hotuba ndefu zaidi, akitumia karibu saa 1 na dakika 50, akiizidi rekodi ya Bill Clinton ya hotuba yake ya mwisho mwaka 2000.
BBC





