Staa wa Kaizer Chiefs jela miaka 12, akutwa na Bangi
Sisti Herman
February 26, 2026
Share :

Mamlaka ya Zimbabwe imemhukumu mshambuliaji wa zamani wa Kaizer Chiefs na Black Leopards Brian Abbas Amidu kifungo cha miaka 12 jela.
Mshambuliaji huyo wa zamani alikamatwa karibu na Kwekwe baada ya maafisa wa upelelezi kumpata akiwa amebeba bangi inayoripotiwa kuwa na thamani ya karibu $75,000 mtaani.





