Tanzania na Canada ni leo Kombe la dunia u20
Sisti Herman
September 11, 2026
Share :

Timu ya Taifa Tanzania, Tanzanite Queens, leo inakabiliana na Canada katika mchezo wa Kombe la Dunia la Wanawake ambao ni lazima washinde, huku wakipambana kuhifadhi matumaini yao ya kusonga mbele hadi hatua inayofuata.
Timu hiyo ya Tanzania imekumbwa na changamoto mwanzoni mwa mashindano hayo yanayofanyika Poland, ikipoteza mechi zake zote mbili za awali katika hatua ya makundi.
Tanzanite Queens ilianza kampeni yake kwa kufungwa mabao 4-1 na Brazil kabla ya kupata kipigo kingine kikubwa cha mabao 5-1 dhidi ya England mnamo Septemba 8.
Kwa sasa Canada ina pointi moja, jambo linalomaanisha kuwa mechi ya mwisho ya hatua ya makundi kwa Tanzania inaweza kuwa ya kuamua hatima ya timu hizo katika kusonga mbele.
Bila pointi yoyote kutoka kwenye mechi zake mbili za awali, sasa Tanzania inahitaji ushindi dhidi ya Canada ili kujipa nafasi ya kufuzu kwa hatua inayofuata.





