Tanzia. Dida Shaibu wa Wasafi afariki Dunia.
Joyce Shedrack
October 5, 2024
Share :
Mtangazaji mkongwe wa Kituo cha Wasafi FM, Dida Shaibu amefariki dunia na mfanyakazi mwenzake wa kituo hicho Maulid Kitenge amethibitisha taarifa za kifo hicho.
Marehemu Dida alikuwa anafanya kipindi cha Mashamsham ndani ya kituo hicho na amefariki katika Hospital ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.
Msiba wa Dida upo nyumbani kwao Sinza na atazikwa leo saa kumi kamili jioni katika makaburi ya kisutu.