Tanzia:Bwege afariki Dunia.
Joyce Shedrack
March 30, 2026
Share :
Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kilwa Kusini Seleman Bungara (Bwege) amefariki Dunia mchana huu, akiwa kwenye Hospitali ya E.M Kigamboni.
Enzi za uhai wake marehemu Bwege amewahi kutumikia vyama vya siasa vya CUF, ACT Wazalendo na hivi karibuni alitangaza kujiunga na CHADEMA, ingawa mchakato rasmi wa kukabidhiwa kadi ya chama hicho ulikuwa haujakamilika.





