Tarehe ya kuachiwa huru kwa Diddy Combs yasogezwa mbele tena.
Joyce Shedrack
August 5, 2026
Share :
Tarehe inayotarajiwa ya kuachiwa huru kwa rapa Sean “Diddy” Combs imesogezwa tena mbele baada ya kuripotiwa kuhusika katika ugomvi akiwa gerezani.
Kwa mujibu wa taarifa za Federal Bureau of Prisons, sasa Diddy anatarajiwa kuachiwa huru Februari 20, 2028. Mabadiliko hayo yamekuja siku chache tu baada ya tarehe yake ya kuachiliwa kubadilishwa kutoka Juni 2028 na kusogezwa mapema hadi Januari 2028.
Bado mamlaka hazijatoa maelezo ya kina kuhusu tukio la ugomvi huo kilisababishwa na nini.





