pmbet

Thamani ya jumba la Shah Rukh Khan yafikia shilingi Bilioni 82.2

Eric Buyanza

July 25, 2026
Share :

Miaka kadhaa kabla ya kuwa mojawapo ya nyumba maarufu zaidi nchini India, nyumba ya ghorofa moja inayotazamana na bahari ilimvutia sana nyota wa filamu nchini India, Shah Rukh Khan, wakati huo alikuwa akirekodi filamu yake ya *Yes Boss* na alijiahidi mwenyewe kuwa siku moja nyumba hiyo ingekuwa yake.

 

Mnamo mwaka wa 2001, ahadi hiyo ilitimia alipoinunua nyumba hiyo ya kifahari kwa thamani ya ₹18 crore (sawa na shilingi Bilioni 4.93 za Kitanzania) na kuliita jumba hilo *Mannat*.

 

Leo hii, makazi hayo maarufu jijini Mumbai yanakadiriwa kuwa na thamani ya takriban rupia bilioni 3 (sawa na shilingi Bilioni 82.2 za Kitanzania), jambo linaloifanya kuwa mojawapo ya nyumba za watu mashuhuri zenye thamani kubwa zaidi nchini humo.

 

Zaidi ya thamani yake ya kifedha, *Mannat* inasimama kama ishara ya azma, uvumilivu, na safari ya kipekee ya mtu aliyebadilisha ndoto kuwa mafanikio makubwa yanayoonekana.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet