Timu 7 za Afrika zimefuzu hatua ya 32 bora bado DRC na Algeria.
Joyce Shedrack
June 27, 2026
Share :
Timu 7 kutoka bara la Afrika zimefanikiwa kufuzu hatua ya 32 Bora kwenye michuano ya Kombe la Dunia 2026 mpaka sasa huku Algeria na DR Congo zikiendelea kupigania nafasi zao katika mechi za mwisho za makundi.

Timu za Afrika zilizofuzu hadi Hatua ya 32 Bora (Round of 32) hadi sasa:
Morocco
Afrika Kusini
Ivory Coast
Ghana
Misri
Cape Verde
Senegal
Algeria inahitaji alama moja dhidi ya Austria katika mchezo utakaopigwa alfajiri ya leo ili kufikisha alama 4 zitakazomuwezesha kufuzu huku DR Congo ikihitaji ushindi dhidi ya Uzbakistan kwenye mchezo wa mwisho ili kufuzu.





