pmbet

Trump atishia kulipua mitambo ya umeme na madaraja ya Iran

Eric Buyanza

July 15, 2026
Share :

Rais wa Marekani Donald Trump amesema jeshi lake litalenga mitambo ya kuzalisha umeme na madaraja nchini Iran wiki ijayo ikiwa Tehran haitarejea kwenye meza ya mazungumzo.

 

Akizungumza katika mahojiano na kituo cha Fox News, Trump amesema hatua hiyo itachukuliwa iwapo Iran haitakubali kuendelea na mazungumzo.

"Ikiwa Iran haitarejea kwenye meza ya mazungumzo, tutalenga mitambo yao ya umeme na madaraja wiki ijayo," alisema Trump.

 

Alipoulizwa kuhusu uwezekano wa kuanzisha operesheni ya vikosi vya ardhini, Trump hakutoa jibu la moja kwa moja.

 

"Sitazungumzia hilo kwa undani. Wakati mwingine operesheni ya ardhini inahitajika, lakini kuna watu wengine watakaoitekeleza kwa niaba yetu," alisema.

Kauli hiyo imekuja wakati mvutano kati ya Marekani na Iran ukiendelea kuongezeka, huku pande zote zikiendeleza mashambulizi na vitisho vya kijeshi.

 

BBC

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet