Trump kuhudhuria fainali ya kombe la dunia na kukabidhi kombe
Eric Buyanza
June 24, 2026
Share :
Rais wa FIFA Gianni Infantino amethibitisha mipango ya kumjumuisha Rais wa Marekani Donald Trump katika hafla ya kukabidhi kombe katika fainali ya Kombe la Dunia.
"Bila shaka tutakuwa pamoja na rais, kufurahia fainali, na kukabidhi kombe kwa mshindi" Infantino alisema wakati wa mahojiano na Fox News.
Itakumbukwa Trump alishiriki katika hafla kama hiyo kwenye fainali ya Kombe la Dunia la Vilabu mwaka jana, wakati Chelsea ilipoilaza Paris Saint-Germain 3-0.






