Tunisia taabani yagaragazwa 5–1 na Sweden
Eric Buyanza
June 15, 2026
Share :

Tunisia wamepata kipigo cha mabao 5–1 kutoka kwa Sweden katika mchezo wao wa kwanza wa Kombe la Dunia 2026, ulioshuhudia makosa mengi ya kiulinzi yakigharimu timu hiyo ya Afrika.
Sweden walitangulia mapema katika dakika ya saba kupitia Yasin Ayari, aliyenufaika na makosa ya beki wa Tunisia baada ya kipa Mouhibb Shamach kupiga mpira uliorudishwa vibaya. Ayari alipiga shuti kali lililoingia wavuni na kuwapa utangulizi Sweden.
Baada ya bao hilo la mapema, Sweden waliendelea kutawala mchezo huo na kuongeza mabao mengine kupitia Viktor Gyökeres, Alexander Isak na Mattias Svanberg.
Tunisia walipata bao lao pekee kupitia Rekik, lakini hawakuweza kurudi mchezoni kutokana na makosa ya mara kwa mara ya safu yao ya ulinzi yaliyozidi kuwapa nafasi Sweden kuendelea kushambulia.





