pmbet

Tuondokane na kadi nyingi zinavimbisha suruali - Mbunge

Eric Buyanza

May 17, 2025
Share :

Mbunge wa Singida Mashariki (CCM), Miraji Mtaturu amesema utekelezaji wa mradi wa Tanzania kidigitali utasaidia mifumo kusomana na kuondokana na watu kutembea na kadi nyingi zinazovimbisha suruali. 

Mtaturu ameyasema hayo bungeni leo alipokuwa akichangia mjadala wa bajeti ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 2025/26.

“Huu ni mwelekeo wa kwenda kwenye e-card tuachane na mtu kuwa na makadi mengi hadi yanavimbisha suruali kumbe huna fedha una makadi mengi mara ya NHIF, leseni, kitambulisho cha kura, huna fedha unakuwa umejaza makadi mengi, ikienda ikapatikana e-card tutaondokana adha hii,”amesema.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet