Tutakaa chini ya shingo ya Arsenal, akifanya kosa tulitumie - Guardiola
Eric Buyanza
February 9, 2026
Share :
Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola, amedokeza kwamba mchezo wao dhidi ya Arsenal unaweza kuamua ubingwa.
Guardiola anaamini wanachohitaji kufanya ni kwenda sambamba na vijana wa Mikel Arteta na kusubiri viongozi hao wa ligi wateleze.
"Tunachoweza kufanya ni kupumua chini ya shingo ya Arsenal, na kujaribu kuona kama watateleza, kama watafanya kosa, tulitumie," alisema.
"Tutawachezea nyumbani, na lazima tuwashinde."






