Urusi yasema imezisambaratisha Droni 635 za Ukraine
Eric Buyanza
August 3, 2026
Share :

Wizara ya Ulinzi ya Urusi imetangaza mapema Jumapili kwamba mifumo ya ulinzi wa anga imezuia na kuharibu ndege zisizo na rubani 635 katika moja ya mashambulizi makubwa zaidi ya ndege zisizo na rubani za Ukraine katika siku za hivi karibuni.
Kulingana na wizara, ndege hizo zisizo na rubani ziliangushwa katika maeneo mengi magharibi na kusini-magharibi mwa Urusi, pamoja na katika Bahari ya Azov na Bahari nyeusi.
Shambulio hilo katika eneo la Saratov limesababisha vifo viwili na uharibifu wa miundombinu. Ripoti za kiwanda cha kusafishia mafuta kushambuliwa bado hazijathibitishwa.
RFI





