Van Persie atabaki Feyenoord licha ya matokeo mabaya
Eric Buyanza
March 10, 2026
Share :
Uongozi wa klabu ya Feyenoord umeamua kumuunga mkono kocha wao, Robin van Persie, baada ya mashabiki wa timu hiyo kumshambulia mwishoni mwa wiki.
Van Persie alikabiliwa na mashabiki hao baada ya timu yake kupata sare ya 3-3 dhidi ya NAC Breda, na wengine wakimtaka ajiuzulu.
Uamuzi wa Feyenoord kumuunga mkono Van Persie unakabiliwa na changamoto kubwa, kwani timu hiyo imepata matokeo mabaya hivi karibuni ikiwa ni pamoja na kufungwa na Heerenveen kwenye Kombe la KNVB.






