pmbet

Vita vyasababisha uhaba wa pombe Saudi Arabia

Eric Buyanza

May 2, 2026
Share :

Duka pekee la serikali la pombe nchini Saudi Arabia linakabiliwa na upungufu wa bidhaa mbalimbali, kuanzia bia na mvinyo hadi tequila, huku wateja wakiiambia Reuters kuwa usambazaji umechelewa kutokana na athari za vita vya Iran.

 

Duka hilo lililopo katika eneo la kidiplomasia mjini Riyadh linafanya kazi bila jina wala bango la kunadi biashara.

 

Lilifunguliwa mwaka 2024 kuhudumia mabalozi wasio Waislamu, na mwaka uliopita likapanua huduma zake kwa wafanyakazi matajiri wasio Waislamu kutoka nje ya nchi.
 

Hata hivyo, marufuku kamili ya matumizi ya pombe iliyoanza kutumika mwaka 1952 bado yanaendelea nchini Saudi Arabia. Licha ya msimamo wake wa kihafidhina, taifa hilo limeruhusu duka moja lenye leseni kwa lengo la kuvutia wafanyakazi wa kigeni.
 

Kwa mujibu wa Reuters, watu watano waliolitembelea duka hilo siku za hivi karibuni walisema rafu zake zilikuwa na bidhaa kidogo za pombe, ambazo ni ghali na zingine za kampuni zisizojulikana sana.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet