Vozinha apata timu Chile
Sisti Herman
July 26, 2026
Share :

Kipa aliyetamba dhidi ya Argentina na Hispania kwenye kombe la dunia Vozinha ameripotiwa kuwa mbioni kusaini mkataba na klabu ya Colo Colo ya ligi kuu nchini Chile kama kipa mpya wa klabu.
Kwa mujibu wa Fabrizio Romano, Makubaliano kati ya pande mbili, mchezaji na timu yamefikiwa na Vozinha atasafiri kwenda Chile mapema wiki ijayo ili kuwa kipa mpya wa Colo Colo.
Mkataba umeshaandaliwa na nyaraka zinatarajiwa kusainiwa, ambapo Colo Colo itamtambulisha shujaa huyo wa Cape Verde kama mchezaji wao mpya.





