"Wa Morocco nawapenda lakini hii ni aibu kubwa kwa soka la Afrika"-Evra.
Joyce Shedrack
March 18, 2026
Share :
Gwiji wa Manchester United na Juventus Patrice Evra amefunguka kuhusu uamuzi wa Kamati ya Rufaa ta CAF kuinyang’anya Timu ya Taifa ya Senegal ubingwa wa AFCON 2025 na kuipatia Timu ya Taifa ya Morocco huku akikiri ni aibu kubwa kwa soka la Afrika.

“Hii ni aibu kwa soka la Afrika. Kashfa kabisa sote tuliona kwa macho yetu kwamba Senegal walishinda".
"Ndugu zangu wa Morocco, nawapenda, lakini kuna wakati mambo hayawezi kufikishwa hivi, jamani AFCON imepoteza kabisa uaminifu wake.
Nilipopata taarifa, nilidhani ni mzaha".
"Hakuna kinachonishangaza tena kwenye soka, na ndiyo maana nalifuatilia kidogo kwa sababu maamuzi kama haya ni kashfa.” Amesema Evra.





