Wananchi wamepageuza KMC Complex machinjioni.
Joyce Shedrack
March 30, 2026
Share :
Klabu ya Yanga ndo timu inayoongoza kupata ushindi mara nyingi zaidi wakiwa nyumbani kwenye michezo ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu huu mpaka sasa.

Yanga wamepata ushindi wakiwa nyumbani mara 7 kati ya michezo 8 waliyocheza wakiwa nyumbani huku wakitoa sare mchezo mmoja pekee dhidi ya Simba waliocheza kwenye uwanja wa New Amaan Complex.
Simba,Pamba Jiji na Mtibwa ndio wanaofuatia kwenye orodha hiyo huku Mbeya City ikiwa timu pekee ambayo haijapata ushindi nyumbani mpaka sasa.





