Wanaoshirikiana na Israel wanapaswa kuwajibishwa - Iran
Eric Buyanza
May 14, 2026
Share :

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, ameibua hisia kali kufuatia taarifa za ziara ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, nchini United Arab Emirates, akisema hatua hiyo ilikuwa tayari imefahamika na vyombo vya usalama vya Iran muda mrefu uliopita.
“Netanyahu sasa ameweka hadharani kile ambacho taasisi za usalama za Iran zilikuwa tayari zimewasilisha kwa viongozi wetu,” Araqchi amesema.
Katika kauli kali zinazoonekana kuelekezwa kwa UAE na mataifa mengine ya Ghuba, Araqchi amesema:
“Uadui dhidi ya taifa kubwa la Iran ni kamari ya kipumbavu, na ushirikiano au njama na Israel katika mwelekeo huo hauwezi kusameheka. Wale wanaoshiriki kushirikiana na Israel kuleta mgawanyiko wanapaswa kuwajibishwa.”
Kauli hiyo imekuja wakati taarifa kuhusu ziara ya siri ya Netanyahu nchini UAE wakati wa vita dhidi ya Iran zikiendelea kuzua mjadala mkubwa wa kimataifa.
Katika siku za hivi karibuni pia, vyombo vya habari vya Marekani vimeripoti madai kuhusu mashambulizi ya siri ya kijeshi yaliyofanywa na UAE pamoja na Saudi Arabia dhidi ya Iran, taarifa ambazo zimevuta uangalizi mkubwa katika eneo la Mashariki ya Kati.
BBC





