pmbet

Watakaofaulu masomo ya sayansi kusomeshwa BURE - Prof. Mkenda

Eric Buyanza

May 30, 2024
Share :

Serikali imesema wanafunzi 700 watakaofaulu vizuri masomo ya sayansi na wakihitaji kusoma vyuo vya hapa nchini, watasomeshwa bure. 

Aidha, wanafunzi watakaosoma masomo ya sayansi, uhandisi, Tehama, elimu tiba na hisabati hawatakuwa na gharama za kulipia, kwamba serikali itawagharamia kila kitu.

Hayo yalisemwa juzi na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda wakati akizindua maadhimisho ya elimu, ujuzi na ubunifu yaliyofanyika kitaifa katika Mkoa wa Tanga.

“Siyo mikopo, serikali itakulipia gharama zote ikiwamo kujikimu, malazi na chakula mpaka umalize kusoma, ili mradi waendelee kufanya vizuri kwenye masomo yao kwenye vyuo wanavyosomea,” alisema Prof. Mkenda.

Vilevile alisema kupitia ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imeelekeza kuendeleza sayansi na teknolojia na Rais Samia Suluhu Hassan aliagiza zitengwe fedha kwa ajili ya kuwasomesha vijana wanaofanya vizuri katika masomo ya sayansi.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet